Mchakato wa uandikishwaji wa watu katika daftari la kupiga
kura.
Ikiwa zimebaki siku chache kabla ya upigaji wa kura katika
uchaguzi wa serikali za mitaa 2019,Mhe.Selemani S.Jaffo(Mb) na waziri wa
TAMISEMI ametoa rai kwa wananchi wote kutumia vizuri muda uliowekwa wa siku
saba kuanzia tarehe8-14/10/2019 kuhakikisha wanajiandikisha kwenye orodha ya
daftari la wapiga kura ili kupata haki yao ya msingi wa kushiriki kuwapigia
kura wagombea wao.
Pia ameweza kueleza sababu za msingi ikiwepo ni kupata haki
ya msingi kama raia wa Tanzania na licha kupata haki ya msingi vilevile
ukijiandikisha utaweza kugombea nafasi za uongozi katika ngazi ya serikali za
mitaa.
0 Comments