Mapenzi Ni Pesa ?

Mapenzi pesa ni swala amabalo limeteka vichwa vya habari katika mahusiano ya wengi. Wengi hulalama ya kuwa hakuna mapenzi bila ya kuwa na pesa wengine wakisema tafuta pesa mapenzi yatakuja. Ni jambo linalochanganya wengi hata kwa wanaotoa ushauri wa mapenzi nao wamekua wahanga wa swala hili.

Ni kweli mapenzi pesa?
Pesa yaweza kuwa kichocheo mojawapo ya kulifurahia penzi lenu kwa upande mmoja au mwengine. Mfano kuna vizawadi vya ghafla ambavyo wapenzi wengi hupenda kufanyiana na mituko ya hapa hapa na pale. Ila ukweli wa mambo unasema mapenzi yamegawanyika katika pande mbili mapenzi ya dhati na yasiyo ya dhati.
o  MAPENZI YA DHATI:

Wengi ambao wana mapenzi ya dhati swala la pesa limekuwa likishika nafasi ndogo sana(minor) kwa maana hata isipokuwepo waweza furahia na kudumisha mapenzi yao katika ustadi wa hali ya juu.
o  




         #MAPENZI YASIYO YA DHATI:
Wengi huyapenda mapenzi ya kuigiza kiupande ambao utahisi unamteka mwenza wako kiakili na kutambua kuwa unampenda ila la hasha! Huna ata moja unalomuwazia Zaidi ya udanganyifu tu.Katika sekta hii pesa imekuwa ni silaha tosha ya kudumu na mwenza wako